Soma Biblia Kila Siku Juni 2021Sample

Kila mtu atatiwa chumvi kwa moto (m.49). Chumvi ni neno la Yesu. Kwa kulisikia neno hilo mtu ataokoka, atampata Roho Mtakatifu moyoni mwake. Sasa kuokoka kunafanyika kwa moto, yaani kwa utakaso. Utakaso huu Roho Mtakatifu anaufanya kwa nguvu ya neno la Yesu, kama ombi la Yesu katika Yn 17:17 linavyoonyesha: Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli. Mtu anapata uchungu moyoni mwake kutokana na dhambi zake. Anatambua kuwa amemkosea Mungu. Hali hii inamfanya atubu, akiziungama dhambi zake na kuziacha kwa Yesu. Ni maana ya habari za m.43-48 kuhusu kukata mkono na mguu, na kuling’oa jicho na kulitupa! Tutubu lile linaloifanya mikono yetu kutukosesha! Lazima tuishi maisha ya toba. Kwa sababu kila mtu atatiwa chumvi kwa moto. Chumvi ni njema; lakini chumvi ikiwa si chumvi tena, mtaitia nini ikolee? Mwe na chumvi ndani yenu, mkakae kwa amani ninyi kwa ninyi (m.49-50).
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Juni 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Marko na Ezekieli. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Related Plans

Everyday Prayers for Christmas

The Holy Spirit: God Among Us

Sharing Your Faith in the Workplace

Simon Peter's Journey: 'Grace in Failure' (Part 1)

Reimagine Influence Through the Life of Lydia

Positive and Encouraging Thoughts for Women: A 5-Day Devotional From K-LOVE

Never Alone

Gospel-Based Conversations to Have With Your Preteen

The Bible in a Month
