Soma Biblia Kila Siku Juni 2021Sample

Hili ni neno kwako uliye na mali. Yesu anakuonya na kukuita! Kuna mtu aliyemjia Yesu kwa heshima ili apate kujua njia ya kupata uzima wa milele. Alikuwa na mali nyingi. Yesu hakutaka kumpendeza tu, bali kumpa jibu la kweli! Baada ya kuongea naye juu ya amri za Mungu, Yesu akatambua kuwa alikuwa anaitegemea na kuipenda mali yake kuliko Mungu. Kwa hiyo tunasoma katika m.21-22: Yesu akamkazia macho, akampenda, akamwambia, Umepungukiwa na neno moja. Enenda, ukauze ulivyo navyo vyote, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate. Walakini yeye akakunja uso kwa neno hilo, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi. Hivyo Yesu alimsisitizia amri kuu: Usiwe na miungu mingine ila mimi (Kut 20:3)! Je, hazina yako iko kwa Mungu? Zingatia Mt 6:19-21, Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba; bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi; kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Juni 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Marko na Ezekieli. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Related Plans

Everyday Prayers for Christmas

The Holy Spirit: God Among Us

Sharing Your Faith in the Workplace

Simon Peter's Journey: 'Grace in Failure' (Part 1)

Reimagine Influence Through the Life of Lydia

Positive and Encouraging Thoughts for Women: A 5-Day Devotional From K-LOVE

Never Alone

Gospel-Based Conversations to Have With Your Preteen

The Bible in a Month
