Soma Biblia Kila Siku Januari/2022Sample

Sura hii yote inahusu namna Isaka alivyompata mke wake. Ni masimulizi mazuri sana ya kupendeza. Hata katika hatua hii ya maisha ya Ibrahimu Mungu yumo. Tuendelee kujifunza kutokana na imani yake! 1. Kwa sababu ya imani alibarikiwa na Bwana katika vitu vyote (m.1, Bwana alikuwa amembariki Ibrahimu katika vitu vyote). 2. Kwa sababu ya imani alitaka mke wa Isaka awe mcha Mungu (m.3-4, Nitakuapisha kwa Bwana, Mungu wa mbingu, na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke katika binti za Wakanaani ambao nakaa kati yao; bali enenda hata nchi yangu, na kwa jamaa zangu, ukamtwalie mwanangu Isaka mke). 3. Kwa sababu ya imani, lazima Isaka abaki Kanaani, na mke wake ahame aje kwake (m.5-8, Ibrahimu akamwambia [yule mtumishi], Ujihadhari, usimrudishe mwanangu huko. Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa katika nyumba ya babangu, … aliniapia akisema, Nitawapa uzao wako nchi hii … yule mwanamke asipokubali kufuatana nawe, basi, utafunguliwa kiapo changu hiki; lakini usimrudishe mwanangu huko.). 4. Kwa sababu ya imani, mpango wa kumwoza Isaka ulifanikiwa sana (m.7, Yeye [Mungu] atampeleka malaika wake mbele yako, nawe utamtwalia mwanangu mke)!
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Januari/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Januari pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa situ husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Mwanzo. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure.
More
Related Plans

UNPACK This...Being a Good Teammate in Life

Living Like Jesus in a Broken World

Positive and Encouraging Thoughts for Women: A 5-Day Devotional From K-LOVE

Overcoming the Trap of Self-Pity

Who Am I, Really? Discovering the You God Had in Mind

Reimagine Influence Through the Life of Lydia

Seasons of Hardship: Live the Jesus Way

16 Characteristics of the God-Kind of Love - 1 Corinthians 13:4-8

Am I Really a Christian?
