Soma Biblia Kila Siku Januari/2022Sample

Hatujui kama Ibrahimu alimwoa Ketura kabla au baada ya kifo cha Sara. Kwa Ketura alipata wana sita zaidi. Hata hivyo ni kwa njia ya Isaka peke yake Mungu alitaka kutimiza ahadi yake ya kumpa Ibrahimu na uzao wake nchi ya Kanaani. Na Ibrahimu aliheshimu mpango huu wa Mungu. Ndiyo maana twasoma kwamba wale wana aliopata kwa Ketura aliwapa zawadi na kuwaondoa wasikae katika nchi ya Kanaani (m.6, Wana wa masuria aliokuwa nao Ibrahimu, Ibrahimu akawapa zawadi, naye akawaondoa katika mahali alipokaa Isaka mwanawe, wakati wa uhai wake). Ila Isaka alirithi mali yake yote, na Mungu akambariki (m.5 na 11, Ibrahimu akampa Isaka yote aliyokuwa nayo … Ikawa, baada ya kufa kwake Ibrahimu, Mungu akambariki Isaka mwanawe)! Imani yake ilizaa matendo!
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Januari/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Januari pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa situ husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Mwanzo. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure.
More
Related Plans

Parables of Grace: Embrace God’s Love for You

Anchored: The Life and Letters of the Apostle Peter

Live Your OWN Life With Conviction

Sundays at the Track

Jesus Is Our "Light of the World"

Made for More

Christosis: Participation in Christ and Imitation of Christ

Love People?!

Move People Through God Alone
