Soma Biblia Kila Siku Januari/2022Sample

Eliezeri alikuwa amemaliza kutoa habari ya safari yake. Ndipo baba na kaka wa Rebeka wakatambua kuwa huo ni mpango wa Bwana, wala hawakumzuia Rebeka kwenda naye (m.50-51, Labani na Bethueli wakajibu wakasema, Neno hili limetoka kwa Bwana, … Tazama, huyo Rebeka yuko mbele yako, umchukue, ukaende zako awe mke wa mwana wa bwana wako, kama alivyosema Bwana). Rebeka mwenyewe naye alikubali (m.58, Wakamwita Rebeka wakamwuliza, Je! Utakwenda na mtu huyu? Akasema, Nitakwenda)! Na Eliezeri alikumbuka sana agizo la Ibrahimu kwamba Isaka hawezi kwenda kukaa mji wa Nahori, bali mke wake lazima aende Kanaani (m.6-7, Ibrahimu akamwambia [yule mtumishi], Ujihadhari, usimrudishe mwanangu huko)! Kwa hiyo walipotaka abaki kwanza siku kumi hakupendezwa. Akaomba aondoke mara moja. Aliogopa kukawia. Na Isaka akampenda Rebeka (m.67, Rebeka, akawa mkewe, [Isaka] akampenda)!
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Januari/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Januari pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa situ husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Mwanzo. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure.
More
Related Plans

Parables of Grace: Embrace God’s Love for You

Anchored: The Life and Letters of the Apostle Peter

Live Your OWN Life With Conviction

Sundays at the Track

Jesus Is Our "Light of the World"

Made for More

Christosis: Participation in Christ and Imitation of Christ

Love People?!

Move People Through God Alone
