Soma Biblia Kila Siku Januari/2022Sample

Jina la huyo mtumishi ambaye Ibrahimu alimtuma ni Eliezeri (15:2). Alikuwa mcha Mungu kama Ibrahimu, na katika kutimiza wajibu wake alimtegemea Mungu. Hakujiamini mwenyewe kwamba ataweza kufanikiwa kwa uwezo wake (m.12-14, 26-27, Akasema, Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Ibrahimu, nakuomba mambo yangu uyajalie yawe heri leo, ukamfadhili bwana wangu Ibrahimu. ... Yule mtu akainama akamsujudu Bwana. Akasema, Na atukuzwe Bwana …)! Eliezeri alikuwa mtu wa maombi. Bila shaka ni jambo ambalo amejifunza kwa Ibrahimu mwenyewe! Ni dalili ya imani iliyo hai. Nasi tufuate mfano wake. Tusimtumikie Bwana kwa kutegemea nguvu zetu, bali kwa kumkabidhi yeye njia zetu! Zingatia hekima ya Sulemani anaposema, Mkabidhi Bwana kazi zako, Na mawazo yako yatathibitika (Mit 16:3).
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Januari/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Januari pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa situ husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Mwanzo. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure.
More
Related Plans

Game Changers: Devotions for Families Who Play Different (Age 13-18)

10 Qualities of Influential Christians

Relationships That Flourish: A 30-Day Devotional on Finding Security in Christ and Growing Healthy Connections

More Than a Dream Coat

Women and Justice

Coming to Life: 30-Day Devotional

In the Mirror of Life: 31 Days of Identity, Purpose, and Gratitude

The Burning Altar - 14 Days of Calling the Church to Pray
