Soma Biblia Kila Siku Juni 2021Sample

Wakati mwingine mzazi hawezi kujua mtoto wake ana haja zipi bila mtoto mwenyewe kutamka. Yesu alijua tayari haja ya yule kipofu kwamba anataka apate kuona. Hata hivyo alimtaka mwenyewe atamke. Vilevile kwetu Wakristo. Baba yetu wa Mbinguni anajua tayari haja zetu zote. Hata hivyo anataka tumwambie ili tupatapo lile tunalohitaji tutambue wazi kuwa yeye ndiye aliyetupa! Ombeni, nanyi mtapewa (Mt 7:7)! Yaani, tusipoomba tutakosa kitu ambacho tungeweza kupata kwa kuomba. Basi, msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu (Flp 4:6-7).
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Juni 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Marko na Ezekieli. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Related Plans

Everyday Prayers for Christmas

The Holy Spirit: God Among Us

Sharing Your Faith in the Workplace

Simon Peter's Journey: 'Grace in Failure' (Part 1)

Reimagine Influence Through the Life of Lydia

Positive and Encouraging Thoughts for Women: A 5-Day Devotional From K-LOVE

Never Alone

Gospel-Based Conversations to Have With Your Preteen

The Bible in a Month
