Somabiblia Kila Siku 3Sample

Kutokana na ishara za Yesu viongozi wa Wayahudi walifadhaika sana: Tukimwacha hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja, watatuondolea mahali petu na taifa letu(m.47-48). Badala ya kunyenyekea na kumkubali Yesu walizidi kushikilia vyeo vyao kwa nguvu (m.49-50, 53 na 57). Kwa njia hiyo wao wenyewe walisababisha Warumi kuja kuharibu mji wao na taifa lao. [Yesu]alipofika karibu aliuona mji [wa Yerusalemu], akaulilia, akisema, Laiti ungalijua, hata wewe katika siku hii, yapasayo amani! Lakini sasa yamefichwa machoni pako. Kwa kuwa siku zitakuja, adui zako watakapokujengea boma, likuzunguke; watakuzingira na kukuhusuru pande zote; watakuangusha chini wewe na watoto wako ndani yako, wasikuachie jiwe juu ya jiwe, kwa sababu hukutambua majira ya kujiliwa kwako(Lk 19:41-44). Unabii huu wa Yesu ulitimizwa baada ya miaka kama 40, yaani mwaka 70 b.K. Zingatia m.52. Ni kwa mataifa yote!
Scripture
About this Plan

SomaBiblia Kila Siku 3 ni mpango mzuri wa kukusaidia kusoma Biblia kwa njia rahisi. Ufafanuzi wa somo la kila siku unakupa mwanga na kiu ya kuendelea kulitafakari Neno la Mungu ukiwa peke yako au pamoja na wenzako.
More
Related Plans

Legacy Lessons W/Vance K. Jackson

You Say You Believe, but Do You Obey?

Awakening Faith: Hope From the Global Church

24 Days to Reflect on God's Heart for Redemption

30 Powerful Prayers for Your Child Every Day This School Year

Sharing Your Faith in the Workplace

Game Changers: Devotions for Families Who Play Different (Age 8-12)

God's Book: An Honest Look at the Bible's Toughest Topics

Rebuilt Faith
