Soma Biblia Kila Siku 11/2024Sample

Kiongozi asiyefuata maagizo ya Mungu ni kipofu naye atawapoteza wote wanaomfuata. Waisraeli walipomfanya Yeroboamu kuwa mfalme, aliwafanya wamwasi Mungu kwa dhambi nyingi. Hata majirani, yaani watu wa Yuda, waliathirika.Watu wa Yuda hawakuyashika maagizo ya Bwana, Mungu wao, lakini walikwenda katika amri za Israeli walizokuwa wamezifanya wenyewe(m.19). Kwa hiyo BWANA alikataa Israeli (= ufalme wa kaskazini) kama taifa, akawatupa wote, wakatekwa na kuwa watumwa.Bwana akakikataa kizazi chote cha Israeli, akawatesa, na kuwatia katika mikono ya watu wenye kuwateka nyara, hata alipokwisha kuwatupa, watoke machoni pake. ... hata Bwana akawaondoa Waisraeli wasiwe mbele zake, kama vile alivyosema kwa kinywa cha watumishi wake wote, manabii. Basi Waisraeli walichukuliwa mateka kutoka nchi yao wenyewe, waende nchi ya Ashuru, hata leo(m.20, 23). Tukitulia na kutafakari tutagundua kuwa tunayosoma hapa yanalingana sana na hali yetu siku hizi, mbele za Mungu. Somo linakusukuma kufanya nini?
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 11/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Kumi na moja pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Mathayo na 2 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Related Plans

Seasons of Hardship: Live the Jesus Way

UNPACK This...Being a Good Teammate in Life

Am I Really a Christian?

Positive and Encouraging Thoughts for Women: A 5-Day Devotional From K-LOVE

Who Am I, Really? Discovering the You God Had in Mind

Overcoming the Trap of Self-Pity

16 Characteristics of the God-Kind of Love - 1 Corinthians 13:4-8

Don’t Know What You’re Doing After Graduation? Good.

Living Like Jesus in a Broken World
