YouVersion Logo
Search Icon

Soma Biblia Kila Siku 06/2024Sample

Soma Biblia Kila Siku 06/2024

DAY 20 OF 30

Ukarimu una baraka zake.Msisahau kufadhili wageni, maana wengine wamewakaribisha malaika wa Mungu pasipo kujua(Ebr 13:2). Mtu na mkewe katika Shunemu walionyesha ukarimu kwa Elisha, nabii wa Mungu, kila alipopita njia ile katika safari zake. Hata walimwandalia chumba. Elisha alipotaka awafanyie kitu kuwaonyesha shukrani, alijulishwa shida yao kubwa: Walikosa mtoto. Ni furaha kuwa na mtoto au watoto katika ndoa, na huzuni kubwa kwa wanandoa ikiwa hawana. Tuwakumbuke katika maombi yetu.

About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 06/2024

Soma Biblia Kila Siku 06/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa sita pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha 2 Timotheo na 2 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu

More