Soma Biblia Kila Siku/ FEBRUARI 2023Sample

Obadia aliishi wakati maadui walipoteka Yerusalemu na kuchukua mali zake. Ana ujumbe juu ya Edomu, kizazi cha Esau.Mungu anakasirikia Edomu na kuahidi kulipiza kisasi, maana walifurahia na hata kushiriki katika kupigwa kwa Yuda. Anaambiwa, Kwa sababu ya udhalimu aliotendwa ndugu yako Yakobo, aibu itakufunika, nawe utakatiliwa mbali hata milele. Siku ile uliposimama upande, siku ile wageni walipochukua mali zake, na watu wa kabila nyingine walipoingia katika malango yake, na kumpa kura juu ya Yerusalemu, wewe nawe ulikuwa kama mmoja wao (m.10-11). Angalia kwa nini Edomu walifanya udhalimu huu juu ya taifa la kindugu, Walidanganywa na kiburi chao (m.3, Kiburi cha moyo wako kimekudanganya)! Tukikosa huruma na unyenyekevu, na pengine kushangilia mateso ya wengine, Mungu atatuhukumu. Tujichunguze kuhusu unyenyekevu. Tumwombe Mungu atuumbie huo.
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku/Februari 2023 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Februari pamoja na maelezo machache ya kukusaidia kuelewa zaidi neno ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Warumi na 1 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu bure
More
Related Plans

Sharing Your Faith in the Workplace

Biblical Wisdom for Making Life’s Decisions

Everyday Prayers for Christmas

Gospel-Based Conversations to Have With Your Preteen

The Holy Spirit: God Among Us

The Bible in a Month

When You Feel Like Roommates: 4 Day Plan to Help You Love (And Like) Your Spouse for Life

Simon Peter's Journey: 'Grace in Failure' (Part 1)

Never Alone
