YouVersion Logo
Search Icon

Soma Biblia Kila Siku/ FEBRUARI 2023Sample

Soma Biblia Kila Siku/ FEBRUARI 2023

DAY 14 OF 28

Somo linaeleza ile imani ni ya namna gani ambayo ilimfanya Ibrahimu ahesabiwe haki! Pia twaambiwa ni imani gani inayotufanya sisi kushinda kesi yetu katika hukumu ya Mungu! Imani ya Ibrahimu ilikuwa imani ya kuamini ahadi ya Mungu, yaani ahadi ile ya kufanya jambo lisilowezekana kabisa kwa uwezo wa kibinadamu.Ibrahimu aliamini kwa kutarajia yasiyoweza kutarajiwa, ili apate kuwa baba wa mataifa mengi, kama ilivyonenwa, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako (m.18)! Na sisi twahesabiwa haki na Mungu kwa imani hii ya kuamini ahadi ya Mungu, kuwa kwa kufa na kufufuka kwa Yesu Kristo dhambi zetu zimeondolewa na mauti imeshindwa. Ni imani ambayo haikuandikwa kwa ajili yake tu kwamba ilihesabiwa kwake; bali na kwa ajili yetu sisi mtakaohesabiwa vivyo hivyo, sisi tunaomwamini yeye aliyemfufua Yesu Bwana wetu katika wafu; ambaye alitolewa kwa ajili ya makosa yetu, na kufufuliwa ili mpate kuhesabiwa haki (m.23-25)!

About this Plan

Soma Biblia Kila Siku/ FEBRUARI 2023

Soma Biblia Kila Siku/Februari 2023 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Februari pamoja na maelezo machache ya kukusaidia kuelewa zaidi neno ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Warumi na 1 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu bure

More