Somabiblia Kila Siku 3Sample

Kutoka kwa Yuda kunamfanya Yesu aseme: Sasa ametukuzwa Mwana wa Adamu, naye Mungu ametukuzwa ndani yake(m.31). Kwa nini? Kwa sababu kukamatwa kwa Yesu kumekaribia sana kutokana na kazi ya Yuda kumsaliti. Na njia ya Yesu kutukuzwa ni kifo cha msalaba. Yesu amenawisha miguu ya wanafunzi wake, na sasa atakwenda kutoa uhai wake kwa ajili yao. Na hutaka wafuate mfano wake: Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi (m.34; ling. 1 Yoh 3:16-18: Katika hili tumelifahamu pendo, kwa kuwa yeye aliutoa uhai wake kwa ajili yetu; imetupasa na sisi kuutoa uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu. Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo? Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli)!
Scripture
About this Plan

SomaBiblia Kila Siku 3 ni mpango mzuri wa kukusaidia kusoma Biblia kwa njia rahisi. Ufafanuzi wa somo la kila siku unakupa mwanga na kiu ya kuendelea kulitafakari Neno la Mungu ukiwa peke yako au pamoja na wenzako.
More
Related Plans

Legacy Lessons W/Vance K. Jackson

You Say You Believe, but Do You Obey?

Awakening Faith: Hope From the Global Church

24 Days to Reflect on God's Heart for Redemption

30 Powerful Prayers for Your Child Every Day This School Year

Sharing Your Faith in the Workplace

Game Changers: Devotions for Families Who Play Different (Age 8-12)

God's Book: An Honest Look at the Bible's Toughest Topics

Rebuilt Faith
