Soma Biblia Kila Siku 02/2025Mfano

Maher-shalal-hash-bazi(8:1, 3) maana yake ni kutekwa haraka na kuangamizwa. Taifa la Israeli lilipoasi, Mungu alikasirika akawa tayari kuwaadhibu. Maana yake ni kwamba kila tunapomwasi Mungu tunajiweka kwenye hatari ya kuangamizwa kiroho na hata kimwili. Shilo kilikuwa ni chanzo kikuu cha maji kwa Yerusalemu. Katika 2 Fal 20:20 tunasoma kwamba Mfalme Hezekiaalifanya birika na mfereji, akaleta maji ndani ya mji. Hivyo kilikuwa ulinzi wa Mungu kwa mji. Kama mtu angekataa maji hayo, alionekana kukataa ulinzi wa Mungu. Ndivyo walivyofanya, tunasoma katika m.6:Wameyakataa maji ya Shiloa yapitayo polepole, na kufurahi kwa ajili ya Resini na huyo mwana wa Remalia. Hapo tujadili, ni kwa namna gani sisi tunakataa ulinzi wa Mungu?
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 02/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Februari pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Zaburi na Isaya. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: somabiblia.or.tz