Soma Biblia Kila Siku/ FEBRUARI 2023Sample

Wewe ujisifuye katika torati, wamvunjia Mungu heshima kwa kuiasi torati? (m.23). Paulo anawakemea Wayahudi. Mungu amewapa mwanga wa pekee katika neno lake (torati), mwanga ambao Mataifa hawana. Kutokana na mwanga huo wao wamepewa wajibu na nafasi ya kuwa viongozi wa vipofu, mwanga wa walio gizani, wakufunzi wa wajinga, walimu wa watoto wachanga, wenye namna ya maarifa na ya kweli katika torati (m.17-20). Lakini mwanga huu usipowafanya waishi katika imani ya kweli, hautawasaidia lolote, kwa maana kutahiriwa kwafaa kama ukiwa mtendaji wa sheria, lakini ukiwa mvunjaji wa sheria kutahiriwa kwako kumekuwa kutokutahiriwa (m.25). Mioyo yao iko mbali na Mungu. Ni wanafiki. Wana alama ya kuwa Wayahudi, lakini wamemwasi Mungu. Yeye ni Myahudi aliye Myahudi kwa ndani (m.29). Swali: Je, sisi tu Wakristo kweli kwa ndani?
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku/Februari 2023 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Februari pamoja na maelezo machache ya kukusaidia kuelewa zaidi neno ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Warumi na 1 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu bure
More
Related Plans

Gospel-Based Conversations to Have With Your Preteen

When You Feel Like Roommates: 4 Day Plan to Help You Love (And Like) Your Spouse for Life

Two-Year Chronological Bible Reading Plan (First Year-January)

Sharing Your Faith in the Workplace

The Bible in a Month

Simon Peter's Journey: 'Grace in Failure' (Part 1)

Never Alone

You Say You Believe, but Do You Obey?

The Holy Spirit: God Among Us
