Soma Biblia Kila Siku/ FEBRUARI 2023Sample

Kwa sehemu Watanzania walimjua Mungu hata kabla wamisionari hawajaileta Injili. Kutokana na dhamiri zao waliweza kujua yaliyo mema na mabaya yaliyoandikwa mioyoni mwao (m.14-15). Na kutokana na uumbaji wa Mungu na matendo yake katika uumbaji waliweza kumtambua. Walijua yu mwema na kwamba huadhibu maovu kwa kuwa mambo ya Mungu yanayojulikana yamekuwa dhahiri ndani yao, kwa maana Mungu aliwadhihirishia (1:19-20). Wabantu walimwita Mungu kwa majina mbalimbali, na baadhi ya mababu walimwamini kweli Mungu na kukataa maovu! Katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye (Mdo 10:3). Kwa uelewa zaidi linganisha na 10:1-5, Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe. Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa. Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu. Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki. Kwa maana Musa aliandika juu ya haki itokayo kwa sheria, ya kuwa, Mtu afanyaye hiyo ataishi kwa hiyo.
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku/Februari 2023 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Februari pamoja na maelezo machache ya kukusaidia kuelewa zaidi neno ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Warumi na 1 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu bure
More
Related Plans

Gospel-Based Conversations to Have With Your Preteen

When You Feel Like Roommates: 4 Day Plan to Help You Love (And Like) Your Spouse for Life

Two-Year Chronological Bible Reading Plan (First Year-January)

Sharing Your Faith in the Workplace

The Bible in a Month

Simon Peter's Journey: 'Grace in Failure' (Part 1)

Never Alone

You Say You Believe, but Do You Obey?

The Holy Spirit: God Among Us
