Soma Biblia Kila Siku Juni 2021Sample

Ezekieli anaagizwa kutabiri hukumu juu ya mfalme wa Misri, nchi yake, na wote walioambatana naye. Farao anafananishwa na joka kubwa mwenye kuonyesha kiburi cha utawala na umiliki wa mto Nile. Mungu anachukizwa na yeyote anayejifanya kuwa Muumba, kama ilivyoelezwa katika m.3 na 9: Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ewe Farao, mfalme wa Misri, joka kubwa aoteaye kati ya mito yake, aliyesema, Mto wangu ni wangu mwenyewe, nami nimeufanya kwa ajili ya nafsi yangu. Hukumu yake juu ya Wamisri itadumu miaka 40, kisha atawarejeza, ila watabaki kuwa duni. Hiyo itakuwa fundisho muhimu kwa watu wa Mungu siku zote: Wasiwategemee watu na mamlaka yao jinsi walivyowahi kufanya: Watu wote wakaao Misri … wamekuwa mwanzi wa kutegemewa kwa nyumba ya Israeli. … nao walipokutegemea, ulivunjika … [ufalme wa Wamisri] hautakuwa tena tumaini la nyumba ya Israeli (m.6b-7 na 16). Tuzingatie kwamba ni heri kumkimbilia Bwana kuliko kuwatumainia wanadamu (Zab 118:8).
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Juni 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Marko na Ezekieli. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Related Plans

Reimagine Transformation Through the Life of Paul

House of David, Season 2: Trusting God in the Middle of the Story

Faith in Action: A Journey Through James

How to Love Your Work and God

The Letter to the Philippians

Lighting Up Our City Video 2: Avoiding Insider Language

How Is It With Your Soul?

Honest to God

How to Love Like Jesus
