Soma Biblia Kila Siku 6Sample

Sasa uenezaji wa Injili ulipiga tena hatua muhimu mbele. Atheneni mji mkuu wa Ugriki. Ulikuwa ni kitovu cha falsafa na mahojiano kuhusu dini. Rudia m.19-22:Waathene na wageni waliokaa huko walikuwa hawana nafasi kwa neno lo lote ila kutoa habari na kusikiliza habari za jambo jipya.Paulo akasimama katikati ya Areopago, akasema, Enyi watu wa Athene, katika mambo yote naona ya kuwa ninyi ni watu wa kutafakari sana mambo ya dini. Kabla Warumi hawajawa watawala kuna kipindi ambacho watawala wa dunia walikuwa ni Wagriki. Kwa kipindi hicho lugha yao ilienea sana. Kila mahali alipofika Paulo aliweza kutumia lugha ya Kigriki kama ilivyo kwa Kiingereza siku hizi. Pamoja na lugha yao pia imani yao ilienea sana. Waliamini na kuabudu mchanganyiko wa miungu mingi. Zingatia wito wa m.30-31: Zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni; bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu. Kwa maana ameweka siku atakayowahukumu walimwengu kwa haki, kwa mtu yule aliyemchagua; naye amewapa watu wote uthabiti wa mambo haya kwa kumfufua katika wafu.
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 6 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.
More
Related Plans

Lead Through Prayer

Peace on Earth: A 5-Day Advent Devotional

Transformational Days of Courage for Women

The Book of Psalms (30-Day Journey)

Unapologetically Sold Out: 7 Days of Prayers for Millennials to Live Whole-Heartedly Committed to Jesus Christ

God Says I Am: Embracing Peace & Walking in Power

When You’re Desperate: 21 Days of Honest Prayer

Lost Kings | Steward Like a King

Come Holy Spirit
