Soma Biblia Kila Siku 6Sample

Suala la ubatizo limezungumzwa sana Tanzania. Ni muhimu tusijenge mafundisho ya ubatizo juu ya somo moja tu. Ni lazima tujenge juu ya mafundisho yote ya Agano Jipya ili tuwe na imani safi (Efe 2:20,Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni)! Ukitaka kufuata maneno yale tu yanayopatana na hoja zako hujawa mtii kwa Roho Mtakatifu. Maana yeye aliwaongoza Mitume katika yote waliyoandika (2 Pet 1:20-21, Hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu). Ni kama vile Yesu alivyowaahidi (Yn 14:26,Huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia; Yn 16:13,Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote). Fundisho la leo: Kumpokea Roho Mtakatifu kunakwenda sambamba na ubatizo, yaani, ubatizo wa kikristo: Wakabatizwa kwa jina la Bwana Yesu. Na Paulo, alipokwisha kuweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao(m.5-6).
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 6 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.
More
Related Plans

Lead Through Prayer

Peace on Earth: A 5-Day Advent Devotional

The Lies We Believe: Beyond Quick Fixes to Real Freedom Part 2

FruitFULL - Faithfulness, Gentleness, and Self-Control - the Mature Expression of Faith

Judges | Chapter Summaries + Study Questions

Let Us Pray

Ruth | Chapter Summaries + Study Questions

Faith in Hard Times

Breath & Blueprint: Your Creative Awakening
