Soma Biblia Kila Siku 02/2025Mfano

Isaya alitumika nyakati za utawala wa wafalme wanne. Alipata maono. Mungu anasikitishwa na dhambi za watu wake. Anajisikia kama baba ambaye watoto wake wapendwa wamempa kisogo.Nimewalisha watoto na kuwalea, nao wameniasi(m.2). Amejaribu kuwarudisha, lakini hawataki kuelewa.Israeli hajui, watu wangu hawafikiri.Kwa maumivu mengi moyoni Mungu anawauliza:Mnataka kupigwa hata sasa, hata mkazidi kuasi?(m.3 na 5). Matokeo yake ni kwamba Yuda, Ufalme wa Kusini, ni kama walioachwa. Hata hivyo BWANA ameacha mabaki. Nabii anaona kwamba Mungu asingalifanya hivyo, Ufalme wa Kusini usingalikuwepo kabisa:Bwana wa majeshi asingalituachia mabaki machache sana, tungalikuwa kama Sodoma, tungalifanana na Gomora(m.9). Huruma zake Mungu hazikomi. Nyakati za sasa hufanana na za Isaya. Je, tunafikiri sisi? Maonyo ya Mungu hayabadiliki, na huruma na fadhili zake bado ni nyingi.
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 02/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Februari pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Zaburi na Isaya. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: somabiblia.or.tz