Soma Biblia Kila Siku 06/2024Sample

Paulo aliitwa kuwa Mtume wa Kristo ili aihubiri na kuifundisha Injili yake. Kwa kutii wito alioitiwa, Paulo amepatikana na mateso na kufungwa gerezani. Lakini haionei aibu Injili wala hamlaumu mtu yeyote kwa yaliyompata. Siri ya utulivu huu wa Paulo hata katika vifungo, mateso na dhiki ni nini? Anamjua Yesu! Naye ana uhakika kwamba kwa njia ya Roho Mtakatifu Yesu mwenyewe atamlinda pamoja na kile ambacho Yesu amempa. Hicho ndicho imani, upendo na tumaini kwa wokovu katika Yesu Kristo. Tafakari pia Paulo anavyosema katika Rum 5:3-5:Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi; na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini; na tumaini halitahayarishi; kwa maana pendo la Mungu limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na Roho Mtakatifu tuliyepewa sisi.
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 06/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa sita pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha 2 Timotheo na 2 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Related Plans

24 Days to Reflect on God's Heart for Redemption

30 Powerful Prayers for Your Child Every Day This School Year

Game Changers: Devotions for Families Who Play Different (Age 8-12)

Rebuilt Faith

Sharing Your Faith in the Workplace

Protocols, Postures and Power of Thanksgiving

Legacy Lessons W/Vance K. Jackson

You Say You Believe, but Do You Obey?

God's Book: An Honest Look at the Bible's Toughest Topics
