YouVersion Logo
Search Icon

Soma Biblia Kila Siku 06/2024Sample

Soma Biblia Kila Siku 06/2024

DAY 14 OF 30

Mwanadamu kujaribu kushindana na maamuzi ya Mungu ni hatari. Hakuna anayeweza kushindana na Mungu kisha akashinda. Ahazi alijaribu kushindana na Mungu kwa kutuma askari ili wamkamate Eliya, nabii wa Mungu. Hakutaka kusikia ukweli. Bila shaka alifanya kwa minajili ya kunyamazisha sauti ya Mungu kwa kumwua Eliya. Askari 102 walikufa kabla Ahazi hajatambua kuwa hakuweza kumwua. Je, wewe pia unatafuta kunyamazisha sauti ya Mungu anapokuambia ukweli? Jifunze haiwezekani. Neno la Mungu litatimia.

About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 06/2024

Soma Biblia Kila Siku 06/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa sita pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha 2 Timotheo na 2 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu

More