Soma Biblia Kila Siku Julai 2023Sample

Bwana atawarejeza tena watu wake. Maneno haya yanaashiria kurudi kwa wana wa Yuda katika nchi yao baada ya utumwa wa miaka 70 huko Babeli, na hata watu wa mataifa kuingia katika ufalme wa Mungu kipindi cha kanisa la kwanza.Baada ya mambo haya nitarejea, Nami nitaijenga tena nyumba ya Daudi iliyoanguka. Nitajenga tena maanguko yake, Nami nitaisimamisha; Ili wanadamu waliosalia wamtafute Bwana, Na mataifa yote ambao jina langu limetajwa kwao; Asema Bwana, ajulishaye hayo tangu milele(Mdo 15:16-18). Mungu hana hasira milele. Katika Zab 103:9 twasoma,Yeye hatateta sikuzote, Wala hatashika hasira yake milele.Pia Mungu mwenyewe anasema,Kwa kitambo kidogo nimekuacha; lakini kwa rehema nyingi nitakukusanya(Isa 54:7). Hata sasa anaonesha uvumilivu wake kwa wenye dhambi, na yuko tayari kuwasamehe na kuwapokea tena kwake. Kama unahukumiwa moyoni kuwa mkosa, huu ni ujumbe mzuri kwako. Rudi kwa Bwana wako, atakurudia.
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Julai 2023 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kuelewa somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Kutoka na Amosi Karibu kujiunga na mpango huu.
More
Related Plans

Gospel-Based Conversations to Have With Your Preteen

Never Alone

Simon Peter's Journey: 'Grace in Failure' (Part 1)

Two-Year Chronological Bible Reading Plan (First Year-January)

When You Feel Like Roommates: 4 Day Plan to Help You Love (And Like) Your Spouse for Life

Everyday Prayers for Christmas

The Holy Spirit: God Among Us

Biblical Wisdom for Making Life’s Decisions

Sharing Your Faith in the Workplace
