Soma Biblia Kila Siku Julai 2023Sample

Historia ikiandikwa kwa usahihi, husaidia kuelewa tabia ya wanadamu. Tangu kale wanadamu wamekuwa waovu, na Mungu hakunyamaza kuonya na kuadhibu. Kwa hiyo tunajua Mungu anavyochukia mienendo mibovu. Hii ni hulka ya Mungu. Wadameski, Wafilisti na wakazi wa Tiro walipowadhulumu Waisraeli, Mungu alitamka hukumu kwao. Kwa Wafilisti anasema,Kwa makosa matatu ya Gaza, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu waliichukua katika hali ya kufungwa kabila nzima, wawatie katika mikono ya Edomu; lakini nitapeleka moto juu ya ukuta wa Gaza, nao utayateketeza majumba yake. Nami nitamkatilia mbali mwenyeji katika Ashdodi; na yeye aishikaye fimbo ya enzi katika Ashkeloni; nami nitaugeuza mkono wangu uwe juu ya Ekroni; na mabaki ya Wafilisti wataangamia, asema Bwana MUNGU (m.6-8). Ndiye Mlipa kisasi wa haki.Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana(Rum 12:19). Tujifunze kwambaasiwepo mtu awaoneaye wengine akidhani atakuwa salama.
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Julai 2023 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kuelewa somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Kutoka na Amosi Karibu kujiunga na mpango huu.
More
Related Plans

Gospel-Based Conversations to Have With Your Preteen

Never Alone

Simon Peter's Journey: 'Grace in Failure' (Part 1)

Two-Year Chronological Bible Reading Plan (First Year-January)

When You Feel Like Roommates: 4 Day Plan to Help You Love (And Like) Your Spouse for Life

Everyday Prayers for Christmas

The Holy Spirit: God Among Us

Biblical Wisdom for Making Life’s Decisions

Sharing Your Faith in the Workplace
