Soma Biblia Kila Siku Julai 2023Sample

Musa aliagizwa kuinua mikono yake mbinguni, kukawa na giza nene lililofunika maeneo ya Wamisri kiasi cha hao kushindwa hata kusogea kwenda popote kwa siku tatu. Ili Mungu audhihirishe ulinzi wake, Waisraeli walikaa katika nuru kwenye makazi yao. Kwa mara nyingine Farao anatoa ruhusa kwa masharti yasiyokubalika, na Musa anasisitiza ni lazima kufuata maagizo ya BWANA kikamilifu, akisema,Ni lazima utupe mikononi mwetu na wanyama wa dhabihu na wa sadaka za kuteketezwa, ili tupate kumchinjia Bwana Mungu wetu dhabihu. Makundi yetu pia watakwenda pamoja nasi; hautasalia nyuma hata ukwato mmoja; kwa maana inampasa kutwaa katika hao tupate kumtumikia Bwana, Mungu wetu; nasi hatujui, hata tutakapofika huko, ni kitu gani ambacho kwa hicho inatupasa kumtumikia Bwana(m.25-26). Ghadhabu ya Farao inatishia kumwua Musa. Farao anaamuru,Nenda zako, ujiangalie, usinione uso tena; kwani siku hiyo utakayoniangalia uso wangu utakufa(m.28). Tukiwa katika Kristo, tupo nuruni, na mabaya hayatatupata. MaanaBwana ndiye mlinzi wako; Bwana ni uvuli mkono wako wa kuume. Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku. Bwana atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako. Bwana atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele(Zab 121:5-8).
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Julai 2023 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kuelewa somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Kutoka na Amosi Karibu kujiunga na mpango huu.
More
Related Plans

Gospel-Based Conversations to Have With Your Preteen

Never Alone

Simon Peter's Journey: 'Grace in Failure' (Part 1)

Two-Year Chronological Bible Reading Plan (First Year-January)

When You Feel Like Roommates: 4 Day Plan to Help You Love (And Like) Your Spouse for Life

Everyday Prayers for Christmas

The Holy Spirit: God Among Us

Biblical Wisdom for Making Life’s Decisions

Sharing Your Faith in the Workplace
