Soma Biblia Kila Siku Julai/2022Sample

Litakuwaje neno hili, maana sijui mume? (m.34) Ujumbe wa malaika ulipita akili ya Mariamu. Alishindwa kuelewa, maana kuchukua mimba bila mwanamume haiwezekani kabisa. Jibu la Gabrieli ni kwamba hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu (m.37). Huwa Mungu anapotenda matendo makuu ya kuwaokoa wanadamu, pia hufanya miujiza mikubwa. Ila huu unapita miujiza yote. Maana ni Mungu mwenyewe aliyeshuka kwetu wanadamu. Mwana wake alifanyika mwili (Yn 1:14, Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu). Ni binadamu na Mungu katika mtu mmoja: Yesu! Maneno ya malaika yanaeleza vizuri, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu (m.35).
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Julai/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Julai pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa siku husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Zakaria na Luka. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure
More
Related Plans

Game Changers: Devotions for Families Who Play Different (Age 8-12)

Legacy Lessons W/Vance K. Jackson

Awakening Faith: Hope From the Global Church

Protocols, Postures and Power of Thanksgiving

Rebuilt Faith

God's Book: An Honest Look at the Bible's Toughest Topics

30 Powerful Prayers for Your Child Every Day This School Year

24 Days to Reflect on God's Heart for Redemption

You Say You Believe, but Do You Obey?
