Soma Biblia Kila Siku Julai/2022Sample

Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa (m.21). Neno ”watu wote” linatupa picha ya ukubwa wa huo uamsho. Kwa nini Yesu alibatizwa? Je, alihitaji kuondolewa dhambi? Hapana. Lakini wote waliotangulia kubatizwa waliweza kutangaziwa msamaha wa dhambi kwa sababu moja tu, yaani, Yesu! Yeye ndiye Mwana-kondoo wa Mungu. Alipobatizwa alikubali kuchukua mzigo wa dhambi za wanadamu wote na kujitoa kama sadaka msalabani ili kutupatanisha na Mungu! Mistari ifuatayo inasema zaidi juu ya jambo hili: Yohana alipomwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu (Yn 1:29)! Na Yohana mwingine aliandika, Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki, naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote. … Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu (1 Yoh 2:1-2; 4:10).
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Julai/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Julai pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa siku husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Zakaria na Luka. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure
More
Related Plans

Game Changers: Devotions for Families Who Play Different (Age 8-12)

Legacy Lessons W/Vance K. Jackson

Awakening Faith: Hope From the Global Church

Protocols, Postures and Power of Thanksgiving

Rebuilt Faith

God's Book: An Honest Look at the Bible's Toughest Topics

30 Powerful Prayers for Your Child Every Day This School Year

24 Days to Reflect on God's Heart for Redemption

You Say You Believe, but Do You Obey?
