Soma Biblia Kila Siku Julai/2022Sample

Wakafurahi pamoja naye ... Akaanza kunena akimsifu Mungu (m.58, 64). Neno ”furaha” limetumika mara nyingi katika Injili ya Luka. Tumeshalikuta katika m.14 na 47. Kiini cha furaha ni neema ya Mungu ambalo pia ni jambo tunalolikuta mara nyingi katika injili hii. Kwa mfano, tazama m.30 anaposema, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Kwa hiyo ni furaha ya kumfurahia Bwana kutokana na neema aliyotukirimia. Na neema yake hasa ni kumtuma Mwana wake ili atuokoe! Furaha hii ilipobubujika kwa Mariamu na Zakaria wakatamka maneno mazuri sana juu ya Mungu. Wakasema, Kwa kuwa Mwenye nguvu amenitendea makuu, Na jina lake ni takatifu. Na rehema zake hudumu vizazi hata vizazi Kwa hao wanaomcha (m.49-50).
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Julai/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Julai pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa siku husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Zakaria na Luka. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure
More
Related Plans

Game Changers: Devotions for Families Who Play Different (Age 8-12)

Legacy Lessons W/Vance K. Jackson

Awakening Faith: Hope From the Global Church

Protocols, Postures and Power of Thanksgiving

Rebuilt Faith

God's Book: An Honest Look at the Bible's Toughest Topics

30 Powerful Prayers for Your Child Every Day This School Year

24 Days to Reflect on God's Heart for Redemption

You Say You Believe, but Do You Obey?
