YouVersion Logo
Search Icon

Soma Biblia Kila Siku Juni/2022Sample

Soma Biblia Kila Siku Juni/2022

DAY 11 OF 30

Kristo Yesu ni haki ile itokayo kwa Mungu. Kwa hiyo kumjua yeye, yaani kumwamini Kristo na kutambua uweza wake uliojitukuza katika kufufuka kwake, ni jambo la maana na msingi imara kwetu. Paulo analitamani hilo, na anawaita Wafilipi na sisi tulichuchumilie. Maana kutambua hivyo kwatupatia faida ipitayo faida ya mambo yote yapatikanayo nje ya Kristo. Kila aliye na Kristo kwa njia ya imani, atakubaliwa na Mungu na kuifikia kiyama ya wafu, yaani kupewa uzima wa milele.

About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Juni/2022

Soma Biblia Kila Siku Juni/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Juni pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa siku husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Wafilipi na Mwanzo. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure

More