SOMA BIBLIA KILA SIKU 01/20Mfano

Kwa kuwa Mungu alifahamu nia mbaya ya Mfalme Herode, alimtokea Yusufu kumwambia amchukue mtoto na wakimbilie Misri ili Herode asimwangamize Yesu katika hila yake. Yesu alizaliwa kwa kusudi maalumu la Mungu ili aokoe ulimwengu na dhambi. Yusufu alitii, akakaa Misri mpaka Herode alipokufa, sawa na unabii wa Hos 11:1 ambapo Mungu anasema, Israeli alipokuwa mtoto, nalikuwa nikimpenda, nikamwita mwanangu atoke Misri. Hasira za Herode kwa kutokuweza kumwua mtoto Yesu, zilimfanya awaue watoto wote wa kiume wa miaka miwili kwenda chini huko Bethlehemu. Alisababisha maafa makubwa yaliyosababisha maombolezo makuu, sawa na unabii katika Yer 31:15 ambapo Bwana asema hivi, Sauti imesikiwa Rama, kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake; asikubali kufarijiwa kwa watoto wake, kwa kuwa hawako.
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 01/20 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Mathayo, Kutoka, Zaburi na Isaya. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Anza mwaka wa 2020 kwa kujifunza Neno la Mungu kupitia mpango huu.
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021

Upendo Wa Bure

Soma Biblia Kila Siku Februari 2021

Soma Biblia Kila Siku Mei 2021

Roho Mtakatifu - Tuna Uwezo Wa Kuwaka Moto Au La?

Soma Biblia Kila Siku 11/2020

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Soma Biblia Kila Siku Januari 2021

Soma Biblia Kila Siku Machi 2021
