SOMA BIBLIA KILA SIKU 01/20Mfano

Katika huduma yake, Yohana alitambua kuwa yeye ni mjumbe aliyetangulia tu, maana atakuja mwingine aliye mkuu zaidi. Yesu alipokuja ndiye aliyekamilisha yale aliyoyaeleza Yohana. Yesu alianza kwa kunyenyekea anapokubali kubatizwa na Yohana. Ni tendo la kujitoa wakfu kwa kazi ya kuwakomboa wanadamu. Baada ya Yesu kubatizwa, ubatizo wa Kikristo ulianza ukiashiria mwanzo wa kipindi kipya cha wana wa Mungu. Ubatizo wa Kikristo ni katika jina la Mungu wa Utatu, na pia Yesu alipobatizwa tunaona utatu wa Mungu: Sauti ya Baba inasikika kutoka mbinguni, akimtambulisha Yesu kuwa ni Mwana, na Roho Mtakatifu anakuja juu ya Yesu kwa mfano wa hua.
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 01/20 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Mathayo, Kutoka, Zaburi na Isaya. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Anza mwaka wa 2020 kwa kujifunza Neno la Mungu kupitia mpango huu.
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021

Upendo Wa Bure

Soma Biblia Kila Siku Februari 2021

Soma Biblia Kila Siku Mei 2021

Roho Mtakatifu - Tuna Uwezo Wa Kuwaka Moto Au La?

Soma Biblia Kila Siku 11/2020

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Soma Biblia Kila Siku Januari 2021

Soma Biblia Kila Siku Machi 2021
