SOMA BIBLIA KILA SIKU 01/20Mfano

Yesu alianza kazi yake kwa kupambana na Shetani katika majaribu. Shetani anatumia ujanja wa kutumia Maandiko Matakatifu akijifanya anataka kumsaidia Yesu katika hali aliyokuwa nayo. Hata hivyo, Yesu anamshida Shetani kwa njia ya Neno la Mungu. Kila mara alimjibu, Imeandikwa. Swali muhimu la kujiuliza, sisi tunapojaribiwa au kupitia mambo magumu, ni hili: Je, tunatafuta msaada wapi? Tuwe makini tusikubali ushawishi wa Shetani wala kutii mapenzi yake. Tulitegemee Neno la Mungu tu, ndilo linalotuletea ushindi wa kweli.
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 01/20 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Mathayo, Kutoka, Zaburi na Isaya. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Anza mwaka wa 2020 kwa kujifunza Neno la Mungu kupitia mpango huu.
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021

Upendo Wa Bure

Soma Biblia Kila Siku Februari 2021

Soma Biblia Kila Siku Mei 2021

Roho Mtakatifu - Tuna Uwezo Wa Kuwaka Moto Au La?

Soma Biblia Kila Siku 11/2020

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Soma Biblia Kila Siku Januari 2021

Soma Biblia Kila Siku Machi 2021
