Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Soma Biblia Kila Siku 4Mfano

Soma Biblia Kila Siku 4

SIKU 3 YA 30

Pigo la nane ni nzige. Mungu alijua kabisa kwamba moyo wa Farao ulikuwa mzito. Na tumekwisha jifunza kwamba kusudi la Mungu lilikuwa kuonyesha uweza wake. Farao alishapata nafasi ya kutubu. Ingawa alikuwa amekwisha shindwa kujadiliana na Mungu kuhusu dai lake, akawa anajaribu tena (m.7-11). Jibu la Mungu lilikuwa kuwaleta wale nzige. Hakutaka kujadiliana na Farao. Bali Mungu ndiye aamuruye. Kwa hiyo sisi wa leo tujifunze kwamba tusigeuze neno la Mungu wala kujadiliana na Mungu, bali tufuate maagizo yake!

siku 2siku 4

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 4

Soma Biblia Kila Siku 4 inakupa mpango wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu, hasa kutoka Kitabu cha Kutoka, na 1 Wathesalonike, pamoja na maelezo juu ya somo hilo.

Tungependa kushukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha