Soma Biblia Kila Siku 08/2024Sample

Yosia, Mfalme wa Yuda, aliyaondoa machukizo yote yaliyokuwa ndani ya Yuda. Hapa katika m.24 wanatajwa wenye pepo wa utambuzi, wachawi, vinyago na sanamu zilizokuwa katika Yuda wakati huo:Wenye pepo wa utambuzi, na wachawi, na vinyago, na sanamu, na machukizo yote yaliyoonekana katika nchi ya Yuda na katika Yerusalemu, Yosia akayaondoa yote, ili apate kuyathibitisha maneno ya torati yaliyoandikwa katika kile kitabu alichokiona Hilkia kuhani ndani ya nyumba ya Bwana. Cha ajabu ni kwamba makuhani sio wanaoshughulika na kurudisha ibada za Bwana kwenye utakatifu wake, bali Mfalme Yosia. Ni baraka ya nchi watu wa serikali na kanisa wanaposaidiana kuleta ibada za kweli. Mungu anaweza kukutumia hata wewe kwa utumishi wake. Umruhusu akutakase na akutumie atakavyo.
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 08/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Nane pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha 2 Wafalme na 1 Timotheo. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Related Plans

You Say You Believe, but Do You Obey?

Everyday Prayers for Christmas

The Bible in a Month

Never Alone

Sharing Your Faith in the Workplace

Simon Peter's Journey: 'Grace in Failure' (Part 1)

The Holy Spirit: God Among Us

Two-Year Chronological Bible Reading Plan (First Year-January)

Gospel-Based Conversations to Have With Your Preteen
