Soma Biblia Kila Siku Julai/2022Sample

Vipi na uovu uliotapakaa katika jamii? Maono ya efa (= kikapu) na mwanamke yaonyesha jinsi nchi ya Israeli hatimaye itakuwa huru mbali na ushawishi wa uovu. Shinari ni sawa na Babeli, mahali pa kuabudu sanamu au miungu. Licha ya ibada hizi mara nyingi kuunganishwa na uasherati, zilihesabiwa kuwa uzinzi wa kiroho. Katika Ufu 14:8 imeandikwa, Kisha mwingine, malaika wa pili, akafuata, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli, mji ule ulio mkubwa, maana ndio uliowanywesha mataifa yote mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake. Mfano huohuo wa uzinzi umetumika katika Ufu 17:5, Katika kipaji cha uso wake alikuwa na jina limeandikwa, la siri, BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI. Roho wa Mungu ataangamiza hali hiyo kati ya watu wake. Hatimaye Mungu atatawala uumbaji na taifa lake. Tumwombe atuwezeshe kuutambua uovu huo tusinaswe nao.
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Julai/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Julai pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa siku husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Zakaria na Luka. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure
More
Related Plans

Game Changers: Devotions for Families Who Play Different (Age 8-12)

Legacy Lessons W/Vance K. Jackson

Awakening Faith: Hope From the Global Church

Protocols, Postures and Power of Thanksgiving

Rebuilt Faith

God's Book: An Honest Look at the Bible's Toughest Topics

30 Powerful Prayers for Your Child Every Day This School Year

24 Days to Reflect on God's Heart for Redemption

You Say You Believe, but Do You Obey?
