Soma Biblia Kila Siku 6Sample

Maelezo ya Barnaba na mtume Paulo kuhusu Mataifa kuipokea Injili (habari za ishara na maajabu, ambayo Mungu aliyafanya kwa ujumbe wao katika Mataifa; m.12) hayakuwa tofauti na yale ya mtume Petro: Na Mungu, ajuaye mioyo ya watu, akawashuhudia, akiwapa Roho Mtakatifu vile vile kama alivyotupa sisi; wala hakufanya tofauti kati yetu sisi na wao, akiwasafisha mioyo yao kwa imani(m.8-9). Yakobo, kiongozi wa usharika mama, aliona kuwa haya pia yanapatana na maneno ya manabii wa Agano la Kale. Kwa msingi huu alitoa uamuzi wa suala hilo, kwa sababu Kanisa limejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni(Efe 2:20). Agano jipya la Kristo ni agano la neema. Twaamini kwamba tutaokoka kwa neema ya Bwana Yesu(15:11). Tazama, mimi Paulo nawaambia ninyi ya kwamba, mkitahiriwa, Kristo hatawafaidia neno. Tena namshuhudia kila mtu atahiriwaye, kwamba ni wajibu wake kuitimiza torati yote. Mmetengwa na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa sheria; mmeanguka na kutoka katika hali ya neema. Maana sisi kwa Roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya imani. Maana katika Kristo Yesu kutahiriwa hakufai neno, wala kutokutahiriwa, bali imani itendayo kazi kwa upendo(Gal 5:2-6).
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 6 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.
More
Related Plans

Lead Through Prayer

Peace on Earth: A 5-Day Advent Devotional

The Lies We Believe: Beyond Quick Fixes to Real Freedom Part 2

FruitFULL - Faithfulness, Gentleness, and Self-Control - the Mature Expression of Faith

Judges | Chapter Summaries + Study Questions

Let Us Pray

Ruth | Chapter Summaries + Study Questions

Faith in Hard Times

Breath & Blueprint: Your Creative Awakening
