Injili Ulimwenguni - Sehemu 3Sample

Yesu amponya mama-mkwe wa Petro
Yesu akatoka kwenye sinagogi akaenda nyumbani kwa Simoni. Basi huko alimkuta mkwewe Simoni ana homa kali, nao wakamwomba Yesu amsaidie.
Hivyo Yesu akamwinamia na kukemea ile homa, nayo ikamwacha. Akaamka saa ile ile akaanza kuwahudumia.
Jua lilipokuwa linatua, watu wote waliokuwa na wagonjwa wenye maradhi mbalimbali wakawaleta kwa Yesu, naye akaweka mikono yake juu ya kila mgonjwa, akawaponya.wachafu pia wakawatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele wakisema:
“Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walimjua kuwa yeye ni Kristo.
Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, nao walipomwona wakajaribu kumzuia asiondoke.
Lakini yesu akawaambia, “Imenipasa kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, kwa maana kwa kusudi hili nilitumwa.”
Scripture
About this Plan

Mfuatano huu ni kusanyiko la hadithi kuhusu maisha Kristo itakayoshirikisha watazamaji wote ulimwenguni kwa kutumia mchanganyiko wa kuona na sauti. Maisha na mafundisho ya Yesu yalidhihirishwa katika kitabu hiki cha hadithi ambacho kinafuata masimulizi ya Agano Jipya yanayopatikana katika vitabu vya Injili vya Mathayo, Marko, Luka, na Yohana.
More
Related Plans

The Woman of Faith

Jesus in His Own Words

Find Your Purpose Where You Are

One Minute, One Verse, One Prayer: Truth & Faith

Reading With the People of God #14 Proverbs

A Brighter Future: A 5-Day Devotional

God Gives Good Gifts to Everyone

Overcoming Emotional Overwhelm

Three Cornelias: Navigating Loss With the Bible & Rembrandt
