YouVersion Logo
Search Icon

Plan Info

Injili Ulimwenguni - Sehemu 3Sample

Injili Ulimwenguni - Sehemu 3

DAY 2 OF 7

Yesu aondoa pepo wachafu Kisha Yesu akashuka kwenda kapernaumu, mji wa Galilaya na katika siku ya sabato akawa anafundisha. Wakashangazwa sana na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka. Ndani ya sinagogi palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, akapiga kelele kwa nguvu akisema, "Tuache! tuna nini nawe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ni mtakatifu wa mungu Basi Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akisema, “Nyamaza na umtoke!” Yule pepo mchafu akamwangusha chini yule mtu mbele yao wote, akatoka pasipo kumdhuru. Watu wote wakashangaa wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Kwa mamlaka na nguvu, anawaamuru pepo wachafu, nao wanatoka!” Habari zake zikaanza kuenea kila mahali katika sehemu ile.

Scripture

Day 1Day 3

About this Plan

Injili Ulimwenguni - Sehemu 3

Mfuatano huu ni kusanyiko la hadithi kuhusu maisha Kristo itakayoshirikisha watazamaji wote ulimwenguni kwa kutumia mchanganyiko wa kuona na sauti. Maisha na mafundisho ya Yesu yalidhihirishwa katika kitabu hiki cha hadi...

More

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy