Zaburi 53
53
Mutu asiyemwabudu Mungu
1Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo wa huzuni. Mashairi ya Daudi.
2Mupumbafu anajisemesha hivi katika moyo:
“Hakuna Mungu!”
Wote wamepotoka kabisa,
wametenda mambo ya kuchukiza;
hakuna hata mumoja anayetenda mazuri. #Ang. Rom 3.10-12
3Mungu anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni,
aone kama kuna yeyote mwenye akili
kama kuna yeyote anayemutafuta Mungu.
4Lakini wote wamekosa,
wote wamepotoka pamoja;
hakuna anayetenda mazuri,
hakuna hata mumoja.
5Hao wanaotenda maovu hawajui kitu?
Wanatafuna watu wangu kama mikate;
wala hawajali Mungu.
6Hapo watashikwa na hofu,
hofu ambayo hawajapata kuiona;
maana Mungu ataitawanya mifupa ya waadui,
hao watafezeheka maana Mungu amewakataa.
7Heri ukombozi wa Israeli ungefika kutoka Sayuni!
Mungu atakapotengeneza hali ya watu wake,
wazao wa Yakobo watashangilia;
watu wa Israeli watafurahi.
Currently Selected:
Zaburi 53: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.