Zaburi 53
53
Mutu asiyemwabudu Mungu
1Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo wa huzuni. Mashairi ya Daudi.
2Mupumbafu anajisemesha hivi katika moyo:
“Hakuna Mungu!”
Wote wamepotoka kabisa,
wametenda mambo ya kuchukiza;
hakuna hata mumoja anayetenda mazuri. #Ang. Rom 3.10-12
3Mungu anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni,
aone kama kuna yeyote mwenye akili
kama kuna yeyote anayemutafuta Mungu.
4Lakini wote wamekosa,
wote wamepotoka pamoja;
hakuna anayetenda mazuri,
hakuna hata mumoja.
5Hao wanaotenda maovu hawajui kitu?
Wanatafuna watu wangu kama mikate;
wala hawajali Mungu.
6Hapo watashikwa na hofu,
hofu ambayo hawajapata kuiona;
maana Mungu ataitawanya mifupa ya waadui,
hao watafezeheka maana Mungu amewakataa.
7Heri ukombozi wa Israeli ungefika kutoka Sayuni!
Mungu atakapotengeneza hali ya watu wake,
wazao wa Yakobo watashangilia;
watu wa Israeli watafurahi.
Currently Selected:
Zaburi 53: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Zaburi 53
53
Mutu asiyemwabudu Mungu
1Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo wa huzuni. Mashairi ya Daudi.
2Mupumbafu anajisemesha hivi katika moyo:
“Hakuna Mungu!”
Wote wamepotoka kabisa,
wametenda mambo ya kuchukiza;
hakuna hata mumoja anayetenda mazuri. #Ang. Rom 3.10-12
3Mungu anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni,
aone kama kuna yeyote mwenye akili
kama kuna yeyote anayemutafuta Mungu.
4Lakini wote wamekosa,
wote wamepotoka pamoja;
hakuna anayetenda mazuri,
hakuna hata mumoja.
5Hao wanaotenda maovu hawajui kitu?
Wanatafuna watu wangu kama mikate;
wala hawajali Mungu.
6Hapo watashikwa na hofu,
hofu ambayo hawajapata kuiona;
maana Mungu ataitawanya mifupa ya waadui,
hao watafezeheka maana Mungu amewakataa.
7Heri ukombozi wa Israeli ungefika kutoka Sayuni!
Mungu atakapotengeneza hali ya watu wake,
wazao wa Yakobo watashangilia;
watu wa Israeli watafurahi.
Currently Selected:
:
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.