YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 2

2
Mufalme muchaguliwa wa Mungu
1Kwa nini mataifa yanafanya fujo?
Mbona watu wanafanya shauri la bure? #Ang. Mdo 4.25-26
2Wafalme wa dunia wanajitayarisha,
watawala wanashauriana pamoja
kumwasi Yawe na muchaguliwa wake.
3Wanasema: “Tujiondoe katika utawala wao;
tutupilie mbali minyororo yao!”
4Yule anayetawala juu mbinguni
anawachekelea na kuwazarau.
5Kisha, anawakaripia kwa kasirani
na kuwatisha kwa hasira, akisema:
6“Nimemusimika mufalme niliyemuchagua;
anatawala Sayuni, mulima wangu mutakatifu!”
7Mufalme anasema: “Nitatangaza amri ya Yawe.
Mungu aliniambia: ‘Wewe ni mwana wangu,
mimi leo nimekuwa baba yako. #Ang. Mdo 13.33; Ebr 1.5; 5.5
8Uniombe nami nitakupa mataifa kuwa urizi wako,
na dunia nzima kuwa mali yako.
9Utawaponda kwa fimbo ya chuma,
utawavunja kama chungu cha mufinyanzi!’ ” #Ang. Ufu 2.26-27; 12.5; 19.15
10Sasa, enyi wafalme, mutumie akili;
musikilize onyo hili, enyi watawala wa dunia.
11-12Mumutumikie Yawe kwa woga;
muiname mbele ya mwana wake na kutetemeka,
kusudi asikasirike, nanyi musiangamie kwa rafla;
kwa maana hasira yake inawaka haraka.
Heri wote wanaokimbilia kwake!

Currently Selected:

Zaburi 2: SWC02

Highlight

Copy

Compare

Share

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in