Zaburi 1
1
SEHEMU YA KWANZA
(Zaburi 1–41)
1Heri mutu asiyefuata shauri la waovu,
asiyeshiriki katika njia ya wenye zambi,
wala kukusanyika na wenye kuzarau;
2lakini anafurahia sheria ya Yawe,
na kuifikiri muchana na usiku.
3Huyo ni kama muti uliopandwa kando ya vijito,
unaozaa matunda kwa wakati wake,
na majani yake hayanyauki hata kidogo.
Anafanikiwa katika yote anayofanya.
4Lakini waovu si vile hata kidogo.
Wao ni kama maganda yanayopeperushwa na upepo.
5Kwa hiyo watu waovu wataanguka wakati wa hukumu,
wenye zambi hawatashiriki katika kusanyiko la watu wa haki.
6Maana Yawe anashugulikia njia ya watu wa haki;
lakini njia ya waovu itaangamia.
Currently Selected:
Zaburi 1: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.