Zaburi 14
14
Uovu wa watu
(Ang. Zab 53)
1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.
Mupumbafu anajisemesha hivi katika moyo:
“Hakuna Mungu.”
Wote wamepotoka kabisa,
matendo yao ni ya kuchukiza;
hakuna hata mumoja anayetenda mazuri! #Ang. Rom 3.10-12
2Yawe anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni
aone kama kuna yeyote mwenye akili,
kama kuna yeyote anayemutafuta Mungu.
3Lakini wote wamekosa,
wote wamepotoka pamoja;
hakuna anayetenda mazuri,
hakuna hata mumoja.
4Hao wanaotenda maovu hawajui kitu?
Wanatafuna watu wangu kama mikate,
wala hawajali Yawe.
5Hapo watashikwa na hofu,
maana Mungu ni pamoja na watu wa haki.
6Unaweza kuvuruga mipango ya masikini,
lakini Yawe ndiye kimbilio lake.
7Heri ukombozi wa Israeli ungefika kutoka Sayuni!
Yawe atakapotengeneza hali ya watu wake,
wazao wa Yakobo watashangilia;
watu wa Israeli watafurahi.
Currently Selected:
Zaburi 14: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.