Zaburi 13
13
Kuomba musaada
1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.
2Mpaka wakati gani, ee Yawe,
utaendelea kunisahau?
Mpaka wakati gani utanificha uso wako?
3Mpaka wakati gani
nitakuwa na wasiwasi katika roho
na sikitiko katika moyo siku hata siku?
Mpaka wakati gani waadui zangu watanishinda?
4Uniangalie na kunijibu, ee Yawe, Mungu wangu.
Uyaangazie macho yangu, nisipatwe na usingizi wa kifo.
5Usiwaache waadui zangu waseme: “Tumemushinda huyu!”
Watesaji wangu wasifurahie kuanguka kwangu.
6Lakini mimi ninatumainia wema wako,
moyo wangu ufurahie wokovu wako.
Nitakuimbia wewe, ee Yawe,
kwa vyote ulivyonitendea!
Currently Selected:
Zaburi 13: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.