Zaburi 15
15
Rafiki ya Mungu
1Zaburi ya Daudi.
Ee Yawe,
nani atakayekaa katika hema yako?
Nani atakayeishi juu ya mulima wako mutakatifu?
2-5Ni mutu anayefanya hivi:
anaishi katika ukamilifu,
anatenda kwa haki siku zote,
anasema ukweli kutoka ndani ya moyo,
hatetani,
hatendei rafiki yake uovu,
hamutukani jirani yake,
anazarau wapotevu,
anaheshimu wanaomwabudu Yawe,
hageuzi kiapo chake hata kikimuletea hasara,
hakopeshi feza yake kwa kupata faida,
wala kupokea kituliro kumutesa asiyekuwa na kosa.
Mutu anayefanya vile,
hatatikisika hata kidogo.
Currently Selected:
Zaburi 15: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.