Zaburi 12
12
Kuomba musaada
1Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa vyombo vyenye nyuzi nane. Zaburi ya Daudi.
2Unisaidie,
ee Yawe!
Watu wema wamekwisha;
waaminifu wametoweka kati ya watu.
3Kila mumoja anamudanganya mwenzake;
anabembeleza lakini ni kwa moyo wa unafiki.
4Ee Yawe, ukomeshe midomo hiyo ya kudanganya,
na ndimi hizo zinazojigamba.
5Wao wanasema: “Kwa ndimi zetu tutashinda;
tuko na midomo, nani anayeweza kututawala?”
6Lakini Yawe anasema:
“Kwa sababu wamasikini wanaugua,
na wakosefu wanalia,
sasa ninasimama,
nami nitawapa usalama wanaoutazamia.”
7Ahadi za Yawe ni safi,
safi kama feza iliyosafishwa katika chungu,
kama feza iliyosafishwa mara saba.
8Utulinde, ee Yawe,
utukinge siku zote na kizazi hiki kiovu.
9Waovu wanazunguka popote;
upotovu unatukuzwa kati ya watu.
Currently Selected:
Zaburi 12: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.