Zaburi 11
11
Kumutumainia Mungu
1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.
Yawe ni kimbilio langu;
namna gani basi munaweza kuniambia:
“Ruka kama ndege, mpaka kwenye milima,
2maana waovu wanavuta pinde;
wameweka mishale tayari juu ya kamba,
kusudi wawapige mishale watu wenye moyo wa usawa katika giza!
3Kama misingi ikiharibiwa,
mutu wa haki atafanya nini?”
4Yawe yuko katika hekalu lake takatifu;
kiti cha kifalme cha Yawe kiko mbinguni.
Kwa macho yake anawachungulia wanadamu,
na kujua kila kitu wanachofanya.
5Yawe anawapima watu wa haki na waovu;
anawachukia wanaopenda kutesa kwa ukali.
6Atawanyeshea waovu makaa ya moto na kiberiti;
upepo mukali utakuwa ndio azabu yao.
7Yawe ni wa haki
na anapenda watu watende kwa haki.
Watu wa usawa wataona uso wake.
Currently Selected:
Zaburi 11: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.