YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 11

11
Kumutumainia Mungu
1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.
Yawe ni kimbilio langu;
namna gani basi munaweza kuniambia:
“Ruka kama ndege, mpaka kwenye milima,
2maana waovu wanavuta pinde;
wameweka mishale tayari juu ya kamba,
kusudi wawapige mishale watu wenye moyo wa usawa katika giza!
3Kama misingi ikiharibiwa,
mutu wa haki atafanya nini?”
4Yawe yuko katika hekalu lake takatifu;
kiti cha kifalme cha Yawe kiko mbinguni.
Kwa macho yake anawachungulia wanadamu,
na kujua kila kitu wanachofanya.
5Yawe anawapima watu wa haki na waovu;
anawachukia wanaopenda kutesa kwa ukali.
6Atawanyeshea waovu makaa ya moto na kiberiti;
upepo mukali utakuwa ndio azabu yao.
7Yawe ni wa haki
na anapenda watu watende kwa haki.
Watu wa usawa wataona uso wake.

Currently Selected:

Zaburi 11: SWC02

Highlight

Copy

Compare

Share

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in