Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Mwanamume Wa KifalmeMfano

Mwanamume Wa Kifalme

SIKU 3 YA 5

Kuumbwa Ili Kutawala

Uchunguzi unaonyesha kwamba mngurumo wa simba unaweza kusikika umbali wa maili tano! Mngurumo huu wenye nguvu huinua vumbi kutoka ardhini na kutikisa vitu vilivyoko karibu. Inasababisha kila mnyama kuacha walichokuwa wakifanya na kuchukua tahadhari. Inadai umakini. Kwa nini? Kwa sababu simba hunguruma hivyo akitangaza mamlaka. Anajulisha kila mmoja kwamba wanaingia katika eneo lake, na ana madaraka ya kuwaongoza, kuwatunza na kuwalinda wote walio ndani ya milki yake.

Wanaume mliumbwa kunguruma. Uliumbwa kutawala. Mungu alipomuumba mwanadamu, alimkabidhi shughuli za usimamizi za kila siku. Hadi kufikia wakati huo, Mungu alifanya kazi yote. Alinena na kila kitu kikaumbika, na akapanga kila kitu katika utaratibu wake. Lakini alipomuumba mwanadamu kwenye siku ya sita, alisema, “Watawale.” Sasa kutawala haina maana ya kukandamiza. Badala yake, fikiria kutawala kama kusimamia. Alimpa mwanadamu mamlaka ya usimamizi ili kuilima bustani na kuitunza. Kwa maneno mengine, tunapaswa kuongeza uwezo wa kila kitu katika ulimwengu wetu kwa ajili ya ufalme wa Mungu, na pia tunapaswa kulinda kila kitu katika ulimwengu wetu. Mungu ametupa mamlaka ya kufanya hivyo kwa niaba yake.

Katika kila mchezo wa soka, una wachezaji na viongozi. Wachezaji wana nguvu. Wao ni wachanga, wakubwa, wenye nguvu na wenye kasi zaidi. Wakimpiga afisa, watawaangusha. Viongozi ni wazee, wadogo, dhaifu na pole pole. Na bado, viongozi wanatawala. Wachezaji wanaweza kuwaangusha viongozi, lakini viongozi wanaweza kuwatoa wachezaji nje ya mchezo. Kwa nini? Kwa sababu wana mamlaka. Kamishna wa NFL ametoa mamlaka kwa maafisa kutawala mchezo kwa niaba yake

Wanaume, Mungu ametupa mamlaka ya kutawala kwa niaba yake. Tunatakiwa kutawala uumbaji wa Mungu, lakini ni lazima tufanye kwa njia ya Mungu kwa sababu yeye bado ni mmiliki. Hii ndio maana ya kuwa meneja. Ingawa Mungu ametupa mamlaka, lazima tukumbuke kwamba bado tunaripoti kwake!

siku 2siku 4

Kuhusu Mpango huu

Mwanamume Wa Kifalme

Katika historia yote, Mungu daima amewatafuta na kuwatumia wanaume kuendeleza ajenda ya Ufalme wake. Shetani anajua hili, ndiyo maana anataka kuwafungia na kuwahasi wanaume. Ulimwengu wetu unaendelea ukizorota kwa sababu...

More

Tungependa kuwashukuru The Urban Alternative (Tony Evans) kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://tonyevans.org/

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha