Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Mwanamume Wa KifalmeMfano

Mwanamume Wa Kifalme

SIKU 2 YA 5

Ufafanuzi wa Mwanamume wa Ufalme

Waweza kufafanua vipi uanaume? Baba yako alikufafanulia? Au labda mama yako alifanya hivyo? Vipi kuhusu mkeo? Habari gani marafiki zako? Vipi kuhusu vipindi vya televisheni, sinema na muziki maarufu?Wanawaelezeaje wanaume? Jaribu hili: Funga macho yako, fikiria kuhusu vyanzo hivi vya habari, na uchore picha ya mwanamume akilini mwako.

Je! Unamwona? Anaonekanaje? Je! Anaongea na kujiendesha vipi?

Sasa chukua picha hiyo, ponda ponda iwe mpira, kisha uitupe nje ya dirisha. Puuza kila kitu ambacho kila mtu anasema kuhusu uanaume, na uzingatie ufafanuzi pekee ambao ni muhimu. Huo wa Mungu. Mungu ametufafanulia uanaume, na ametoa picha kamili ya jinsi wanaume wa ufalme wanavyofanana.

Mwanamume wa Ufalme anaweza kufafanuliwa kama mtu anayedhihirisha kwa uwazi utawala kamili wa Mungu chini ya ubwana wa Yesu Kristo katika kila eneo la maisha yake. Asili ya mwanamume wa ufalme inajikita katika upatanisho na utii. Mungu katu hakumtarajia mwanadamu afanye lolote bila kumtegemea Yeye. Tangu mwanzo, alimuumba mwanadamu ili awajibike kwake Kwa mfano, angalia uumbaji wa Adamu. Mungu alimuumba Adamu. Akaumba bustani mahususi kwa ajili ya Adamu na akamuweka humo. Alimpa kazi, kusudi na hatima ya kutimiza. Hatimaye alimpa Adamu maagizo ya kuishi kwayo. Waona, Adamu aliuumbwa kufanya kazi chini ya mamlaka ya kimungu. Hakuumbwa aishi kwa uhuru wake, bali aliumbwa kuchukua mwelekeo kutoka kwa Bwana. Mungu aliumba msururu wa amri, na Adamu alipaswa kuambatana naye ipasavyo.

Gari linapokosa kuwa katika hali ya kufungamana, kuna ishara zinazoonekana: uchakavu wa matairi, safari mbaya nk. Unaweza kuzungusha matairi au kuchezea vidhibiti vya mshtuko, lakini hiyo haitarekebisha tatizo la gari lako. Ndivyo ilivyo na wanaume. Wakati wanaume hawajaunganishwa ipasavyo na Mungu, kunaonekana kuzorota kwa familia, makanisa na jumuiya zetu. Kurudi tu kwenye eneo lako sahihi la upatanishi ndiko kutarekebisha matatizo haya.

siku 1siku 3

Kuhusu Mpango huu

Mwanamume Wa Kifalme

Katika historia yote, Mungu daima amewatafuta na kuwatumia wanaume kuendeleza ajenda ya Ufalme wake. Shetani anajua hili, ndiyo maana anataka kuwafungia na kuwahasi wanaume. Ulimwengu wetu unaendelea ukizorota kwa sababu...

More

Tungependa kuwashukuru The Urban Alternative (Tony Evans) kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://tonyevans.org/

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha