Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Soma Biblia Kila Siku Julai/2022Mfano

Soma Biblia Kila Siku Julai/2022

SIKU 28 YA 31

Luka alianza andiko lake kwa kueleza kuwa nimejitafutia usahihi wa mambo hayo yote tangu mwanzo (1:3). Karibu habari yote ya Lk 1-2 haipo katika injili zile nyingine. Huenda Luka alikuwa ameongea na mama yake Yesu au ndugu zake, k.mf. Yakobo aliyekuwa kiongozi wa usharika mama pale Yerusalemu. Kwa njia hiyo alipata habari kama hii ya leo. Tokea mapema Yesu alijielewa kuwa ni Mwana wa Mungu (taz. m.49). Lakini wazazi wake hawakuelewa sawasawa jambo hili, ingawa malaika alishawajulisha kuwa hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu. … Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake (1:33, 32).

siku 27siku 29

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku Julai/2022

Soma Biblia Kila Siku Julai/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Julai pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa...

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz/

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha